KATIBA MPYA

BUNGE LA KATIBA LAPATA WENYEVITI NA MAKATIBU

Na Naamala Samson,
Baada ya kuendeshwa kwa zaidi ya wiki tatu bila mwenyekiti wa kudumu wala kujadili rasimu ya katiba,sasa bunge maalum la katiba litaanza kujadili vipengele na ibara mbalimbali zilizomo ndani ya rasimu ya katiba kwani wajumbe wa bunge hili muhimu wameweza kufanya uchaguzi na kumchagua Mhe. Samwel Sitta awe Mwenyekiti wa kudumu wa bunge hili kwa muda uliosalia mpaka kupatikana kwa katiba mpya kabla ya katiba hiyo kurudi kwa wananchi kupigiwa kura.
Image
Ikumbukwe kuwa mashirika mengi yalikuwa yanapigia kelele suala zima la wajumbe hawa kutoangalia ubinafsi wao bali kuwaza taifa zima na kutengeneza katiba kwa ajili ya vizazi vijavyo ili Tanzania iwe nchi inayopiga hatua kwa kasi.
By ijuekatiba

ASASI YA VIJANA YA TYVA KUFANYA BARAZA LA KATIBA TAREHE 17 AGOSTI 2013

Image

Dear All,
TYVA is humbly inviting you to attend the Youth Constitutional Council to be held on Saturday 17th August 2013 at Peacock Hotel City Centre Mnazi Mmoja, Dar es Salaam from 08:00am to 4:00pm
The main Goal of the Youth Constitutional Council is to facilitate the collection of youth views on the recently released first draft of constitution, towards the process of writing the new constitution of United Republic of Tanzania.
TYVA will provide breakfast, Lunch Break and all refreshments during the conference. To show your commitment, TYVA request you to cover your own transport to and from the conference at Mnazi mmoja and we will NOT give any transport and sitting allowances to the participants.
Please confirm your participation by sending your Full name to Alfred Kiwuyo by Phone or Email before 14th August, 2013 for farther logistics arrangements. Should you have any questions, please do not hesitate to contact us through the addresses below.
Looking forward to have you on 17th August, 2013
Alfred Kiwuyo, 
Head, Lobbing, Advocacy and Networking (LAN)
akiwuyo@yahoo.ca 
+255 713 618 388 
Tanzania Youth Vision Association
By ijuekatiba

Mhe. Samuel Sitta afungua rasmi Baraza la Vijana la Taifa la Katiba leo jijini Dar es Salaam.

Na Benedict Liwenga.
 
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo Mashiriki, Mhe. Samuel Sitta amewaaasa vijana kutoa maoni yao juu ya uundwaji wa Katiba mpya ambayo haijengi mifumno ya serikli ya Udikteta, ubinafsi na ambayo haitaibebesha mzigo Serikali.
 
Image
 
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mhe. Sitta wakati akifungua rasmi Baraza la Vijana la Taifa la Katiba lililoandaliwa na Taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa kushirikiana na Restless Development, UNFPA na ILO lililojumuisha vijana 120 kutoka Wialaya 50 za mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani na ambao wanatoka katika mashirika mbalimbali, asasi, jumuiya na vikundi mbalimbali vya vijana.
 
Waziri Sitta amewaasa vijana kuwa TYC pamoja na vijana wengine nchini wanalojukumu kubwa la mapambano dhidi ya kupinga ulafi katika mambo ya uongozi, udikteta pamoja na ubinafsi kwani vinailetea mzigo serikali.
 
“Mtu ajue kuwa kutumia madaraka kwa manufaa yako mwenyewe ni mwiko”. Waziri Sitta alisema.
 
Waziri Sitta ameongeza kuwa vijana nchini wanatakiwa wawe Wanaharakati katika kujali maadili mema na kusimamia kwa dhati pamoja na kupigania haki na usawa nchini.
 
Image
 
Aidha, kwa upande mwingine Waziri Sitta amevishukuru vyombo vya habari kwa mchango wake mkubwa wa kufanya kazi ya kuhabarisha umma na npia ameipongeza taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition kwa kuandaa baraza hilo kwa vijana wenzao kwani litawasaidia kutambiua mabo ya msingi yanayohitajika kuwepo katika Katiba mpya ya nchi.
 
Waziri Sitta alisema kuwa katika kutoa maoni juu ya Katiba mpya, vijana wanaweza kupata katiba yenye manufaa mazuri au yenye athari kwa maisha yao, hivyo amewaasa vijana wote watumie fursa wanazozipata kupitia baraza hilo lililoandaliwa na TYC ili waweze kusikika katika mambo yanayohitajika katika Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition ni moja ya taasisi iliyoundwa kwa malengo ya kuhakikisha kuwa vijana wanashirki na kushirikishwa katika mchakato wa kuunda katiba mpya ulioanza mwaka jana hapa nchini.
 
Image
 
By ijuekatiba

VIONGOZI VIJANA WA YLTP 2013 WATOA MAENEO SITA YA KUZINGATIA KWENYE KATIBA

Image
Washiriki vijana katika mjadala kuhusu rasimu ya katiba.
Katika kuendelea na mchakato wa kutoa maoni kuhusu rasimu ya KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vijana wapatao 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, wanaoshiriki mafunzo ya uongozi yanayotolewa na Shirika la Kijerumani la Friedrich Ebert Stiftung(FES) wamefanya mjadala wa siku mbili wa kujadili rasimu hiyo na kutoa maeneo sita wanayoona yanatakiwa kupewa uzito katika kupata katiba mpya.
Maeneo hayo sita ni:
1.Kuimarisha vyombo vya kusimamia uwajibikaji.
2.Suala la umiliki wa Ardhi
3.Usimamiaji na ugawanyaji wa rasilimali.
4.Kutajwa kwa lugha ya kufundishia
5.Kutajwa suala la serikali za mitaa
6.Mfumo mzima wa kubadili katiba hii kwenda mpya.

Comments

UNITEC COMPUTER ACCESS